About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Wednesday, September 21, 2011

MJUMBE WA BODI YA MIKOPO WA SERIKALI ZA MITAA ATEMBELEA SOKO LA SONGEA NA KUJIONEA CHANGAMOTO ZAKE

    Na Amon Mtega,Songea
 
SOKO kuu la Halmashauri ya Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma lililoungua moto mwaka 2003 na kuteketeza kabisa fedha na mali za wafanyabiashara wa soko hilo na kisha kujengwa upya na Manispaa  hiyo kwa fedha zilizotoka kwa wahisani na taasisi za mikopo na kisha kuendelea kutoa huduma hiyo lakini bado linakabiliwa na changamoto mbali mbali.
 
Akitoa taarifa ya uendeshaji wa soko hilo mkuu wa Masoko ya Manispaa ya Songea Salum Homera kwa Mjumbe wa bodi ya mikopo ya Serikali za Mitaa George Mallima Lubeleje alisema kuwa baada ya soko hilo kujengwa upya likiwa na meza 308 na maduka 161 na kwamba linatoa huduma kwa wananchi wa ndani na nje ya mkoa wa Ruvuma.
 
 Alisema kuwa pamoja na huduma hizo halmashauri hukusanya kiasi cha shilingi milioni 9.4 kwa mwezi ambazo hutumika kuisaidia halmashauri kugharamia shughuli mbambali za kiutawala na utoaji huduma kwa wananchi pia serikali kuu hukusanya kodi ya mapato kutoka kwa baadhi ya wafanyabiashara wa soko hilo ambayo huisaidia serikali kutoa huduma boraa kwa wananchi.
 
 Aidha pamoja na mafanikio hayo Homera alisema kuwa zipo changamoto ambazo zinahitaji kutatuliwa ili kuboresha mapato zaidi ikiwemo mahitaji ya ukarabati ambayo ni makubwa kuliko kiasi kinacho kusanywa na soko hilo,baadhi ya wafanyabiashara kuendesha biashara zao nje ya soko na kulikosesha soko mapato na kuchelewa kusainiwa kwa sheria ndogo za halmashauri ambazo huwa zina mapendekezo ya maboresho ya viwango vya kodi na ushuru mbali mbali.
 
 Kwa upande wao wafanyabiashara na wananchi wanaolitumia soko hilo walisema kuwa soko hilo bado linahitaji ukarabati mkubwa ili liweze kuwa na hadhi ya Manispaa na hasa katika maduka ya kuuzia nyama ambako kunahitaji usafi wa hali ya juu tofauti na hali ilivyo sasa.
 
Naye mjumbe wa bodi ya mikopo ya Serikali za Mitaa  George Malima Lubeleje akizungumza baada ya kukagua soko hilo mbali na kupongeza matumizi ya fedha ya mkopo iliyotolewa na bodi hiyo kwa ajili ya ujenzi huo alisema kuwa halmashauri inapaswa kusimamia sheria ndogo ambazo zitasaidia kuongeza kipato na kuweza kumaliza kulipa deni la mkopo huo ili iweze kupewa mkopo mwingine.
 mwisho





No comments:

Post a Comment