About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Thursday, September 22, 2011

CHADEMA WAKATAA KUSIMAMISHA MGOMBEA UMEYA SONGEA





                                     Katibu wa Chadema Jimbo la Songea Masumbuko Paulo
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo(Chadema) wilaya ya Songea  kimemuandikia barua Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea kuhusu dhamira ya chama hicho kutosimamisha mgombea wa nafasi wazi ya Mstahiki Meya wa Manispaa hiyo kutokana na mizengwe na ghiliba zinazofanywa na Mkurugenzi huyo

Akizungumza na waandishi wa habari jana katika ofisi za Chama hicho zilizopo kata ya Mfaranyaki Katibu wa Chadema Jimbo la Songea Masumbuko Paulo alisema kuwa Chama chake kimeamua kutosimamisha mgombea wa kuziba nafasi hiyo kutokana na mizengwe mingi inayoendelea katika harakati za uchaguzi huo

Paulo alisema kuwa Viongozi wa Chadema wamekutana na kutoa msimamo wao kuhusu muenendo huo na kuamua kumjulisha Mkurugenzi wa Manispaa kuwa Chadema hakitasimamisha mgombea katika uchaguzi wa Septemba 23 mwaka huuu

Alisema kuwa Chadema kimemtaka Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea kutopindisha kanuni na sheria kwa maslahi ya Chama Cha Mapinduzi alivyofanya katika uchaguzi uliopita wa kumpata Meya

“Chama kinakukumbusha kufuata kanuni ili kuondoa migongano isiyo ya lazima tena tunamtaadharisha kutoegemea kwa upande mmoja kama unavyofanya sasa”alisema Paulo

Mtandao huu umefanikiwa kuipata barua hiyo ya tarehe 21 Septemba 2011 iliyoenda kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea yenye kumbukumbu namba CH/SMJ/RV/18 yenye kichwa cha habari “Taarifa ya kutosimamisha mgombea wa nafasi wazi ya Mstahiki Meya Manispaa”

Sehemu ya barua hiyo inasomeka “….uchaguzi uliopita wa aina hii haukuwa huru na haki kwani mazingira ya kupiga kura hayakuwa ya siri wala hukuandaa eneo la siri la mtu kupiga kura badala yake ulifanya wajumbe wapiga kura wapige kura ya wajumbe iwe inaonekana kwa wazi tu”

Katika mkutano huo na waandishi Paulo alisema kuwa Chadema ina madiwani 7 ambapo Chama cha Mapinduzi (Ccm) ina madiwani 20 na wabunge wawili kwa maana ya mbunge wa Jimbo la Songea Mjini Dkt Emmanuel Nchimbi,na Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Ruvuma Devota Likokola na kufanya kuwa Ccm iwe na Madiwani 22

Katika uchaguzi huo Ccm imemsimamisha Diwani wa Kata ya Matogoro Charles Mhagama kutokana na Chadema kutomsimamisha mgombea wa kuziba nafasi wazi ya Meya wa Manispaa kunamfanya Charles Mhagama kuwa mgombea pekee wa nafasi

Uchunguzi uliofanywa na mtandao huu umebaini kuwa watu wengi hawajaridhiki na kitendo cha Ccm  kumpitisha Charles Mhagama kuwa mgombea Umeya kutokana na nafasi hiyo kuwa nyeti katika kusukuma mbele gurudumu la maendeleo
Imebainika kuwa baadhi ya madiwani wa Ccm wanamkakati kabambe wa kumpigia kura za hapana mgombea wao ili uchaguzi uhitishwe upya kutokana na Charles Mhagama kutokuwa na mahusiano mazuri na madiwani wezake na kuonekana sio chaguo stahiki

Akizungumza na mtandao huu wa http://www.stephanomango.blogspot.com/ Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea Nachoa Zakaria alikiri kupokea barua ya Chadema na kueleza kuwa kanuni zinaruhusu kufanya uchaguzi ambapo kutakuwa na kura ya ndiyo au hapana

Zakaria alisema kuwa ikiwa wajumbe therusi mbili wakipiga kura za hapana uchaguzi huo utaitishwa upya kwa mujibu wa kanuzi za uchaguzi wa nafasi hiyo ya umeya na kuongeza kuwa uongozi anatoa Mungu na kwamba Halmashauri hiyo inahitaji apatikane Meya na ipo siku atapatikana

Alisema kuwa katika uchaguzi huo atasimamia kikamilifu kanuni na sheria za uchaguzi kwa maslahi ya Halmashauri na wananchi na kudai kuwa madai ya Chadema katika barua yao sio ya msingi kwa kuwa wanalalamikia kitu kilichopita badala ya kuzungumzia uchaguzi uliopo

Uchaguzi huo unafanyika kuziba pengo lililoachwa wazi na marehemu Ally Said Manya aliyefariki Julai 29 mwaka huu katika hospitari ya Misheni ya Peramiho baada ya kuugua muda mrefu maradhi ya moyo na kisukari

AWALI Chadema walimcharukia mgombea wa nafasi ya Umeya wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea kupitia Chama cha Mapinduzi(Ccm) Charles Mhagama kwa madai kuwa sio kiongozi makini na muadilifu anayeweza kulisukuma mbele gurudumu la maendeleo kwa maslahi ya wananchi

Akihutubia mamia ya wakazi wa Manispaa ya Songea  hivi karibuni katika viwanja vya soko la Manzese,kata ya Misufini Mwenyekiti wa chama hicho Mkoa wa Ruvuma Joseph Fuime alisema kuwa nafasi ya Umeya ni nafasi nyeti sana katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea hivyo ina hitaji mtu makini na muadilifu wa kuweza kushirikiana na wadau mbalimbali kuweza kulisukuma gurudumu la maendeleo

Fuime alisema kuwa kutokana na umuhimu huo mgombea aliyepitishwa na Chama cha Mapinduzi (Ccm)Charles Mhagama ili kuweza kuziba nafasi ya Umeya iliyoachwa wazi na Marehemu Ally Manya aliyefariki mwezi julai 29 mwaka huu,kuwa hana uwezo wa kushika nafasi hiyo kutokana na kujaa tamaa ya kujitajirisha kiharamu kupitia fedha za wananchi

Alieleza kuwa Mhagama ni kiongozi mbabe na mwenye kupenda rushwa hali inayodhorotesha maendeleo ya wananchi kwani alishawahi kufanya vitendo viovu ikiwa ni pamoja na kuwepo kwa ushawishi wa rushwa katika ununuzi wa gari ya kuzima moto,uuzwaji wa Katapila la Halmashauri akiwa ni Diwani wa kata ya Matogoro na kiongozi wa Kamati mbalimbali za baraza la madiwani

“Mhagama hawezi kuwa kiongozi bora na atakayeweza kutupeleka kwenye ustawi stahiki wa maisha kwani vitendo vyake vingi ni viovu kwani kuna kipindi alikuwa na mahusiano na mwanafunzi mmoja miaka ya nyuma ambapo alikutwa naye kwenye nyumba ya wageni na wazazi wa mwanafunzi huyo na kupelekewa kupigwa viboko hadharani”alieleza Fuime

Alifafanua kuwa vitendo hivyo vinadhihirisha ni jinsi gain alivyokuwa mchafu na kiongozi mbovu asiyestahili kupewa majukumu makubwa ya Umeya hasa katika kipindi hiki kilichogubikwa na ufisadi,rushwa na urasimu mkubwa Serikalini

Alisema kuwa siku zote Chama cha Mapinduzi kimekuwa kikiwaacha viongozi wazuri na kuwateua viongozi wabovu ili waweze kukinufaisha chama kwa maslahi yao binafsi hivyo hatuwezi kuongozwa na kiongozi wa aina hiyo na ndio maana tunapaza sauti ili umma ujue na kuwaambia Madiwani wao waliowachagua kutokumpigia kura mgombea huyo wa Ccm kwenye uchaguzi wa Serikali unaotegemewa kufanyika Septemba 23 mwaka huu na kuongeza pia Halmashauri ya Manispaa ya Songea ni mali ya wananchi wote na sio mali ya kikundi cha watu wachache wenye malengo yao binafsi
MWISHO

No comments:

Post a Comment