About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Saturday, September 24, 2011

NI AIBU NA FEDHEHA VULUGU ZA UCHAGUZI WA UMEYA SONGEA ! JE NANI WA KULAUMIWA?


 Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini Dkt Emmanuel Nchimbi
 Msimamizi wa uchaguzi Jimbo la Songea Mjini Nachoa Zakaria
 Naibu Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea Mariam Dizumba

Mgombea wa nafasi ya Umeya wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea Charles Mhagama
Na Mwandishi Wetu
MADIWANI wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma wamerushiana makonde baada ya Naibu Meya wa Halmashauri hiyo Mariam Dizumba kudaiwa kuiba kura zilizopigwa na madiwani hao ili kuziba nafasi iliyoachwa wazi ya Mstahiki Meya wa Halmashauri hiyo aliofariki dunia miezi michache iliyopita
Katika uchaguzi huo ulioanza kwa marumbano makubwa yaliyodumu kwa zaidi ya dakika 20 kati ya madiwani wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo(Chadema) na Madiwani wa Chama cha Mapinduzi ambao walikuwa wanajadili namna uchaguzi huo utakavyokuwa  huru na haki kutokana na Chadema kutosimamisha mgombea na Ccm kusimamisha mgombea
Kutokana na hali hiyo Msimamizi wa uchaguzi ambaye pia ni Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Nachoa Zakaria alitoa ufafanuzi wa kanuni za uchaguzi wa nafasi hiyo ambapo aliwataka madiwani kupiga kura za ndio au hapana na kwamba wapigakura halali waliojiorodhesha walikuwa ni Madiwani 26 akiwemo na Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini Dkt Emmanuel Nchimbi
Baada ya hali hiyo kutulia Msimamizi wa uchaguzi Zakaria aliita orodha ya wajumbe na kuwataka wachukue karatasi za kupigia kula ambapo madiwani wote walipiga kura na kuitwa wahesabu kura waweze kuzihesabu kura hizo
Zoezi la kuhesabu kura lilipomalizika Naibu Meya wa Halmashauri hiyo Mariam Dizumba alilisimama na kuanza kutangaza matokeo kwa kudai kuwa Mgombea Umeya wa Halmashauri hiyo Charles Mhagama amepigiwa kura za ndio 14 na kura za hapana 12
Dizumba alisema kuwa kutokana na matokeo hayo namtangaza Diwani wa kata ya Matogoro Charles Mhagama kuwa ndiye Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea kuanzia sasa
“Naomba Msimamizi wa uchaguzi umuite Diwani Mhagama aweze kuvaa joho la Umeya na kukalia kiti chake”alisema Dizumba
Baada ya Msimamizi wa uchaguzi  Zakaria kumuita Diwani Mhagama na kumtaka avue joho la Udiwani na kuvaa joho la Umeya ndipo baadhi ya madiwani walipomtaka Msimamizi wa uchaguzi azihesabu upya kura hizo ili madiwani wote wazione
“Naomba msimamizi usitishe zoezi la kumtaka Diwani Mhagama akalie kiti cha Umeya kwa sababu kuna mashaka makubwa na zoezi la utangazaji wa matokeo yake hivyo zihesabiwe kura upya na madiwani wote wazione”alisema Diwani wa kata ya Mfaranyaki Seneta Yatembo
Jambo ambalo Msimamizi wa uchaguzi alionekana kupata kigugumizi nalo na kumsababisha Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini Dkt Nchimbi kuingilia mgogoro huo na kupelekea kuharibu hali ya hewa na kuanza kurushiana lugha za matusi miongoni mwa madiwani
Wakati mgogoro huo ukiendelea Diwani wa Viti Maalum Chadema Rhoda Komba akaanza kuwaita madiwani wenzake  ili waweze kumuona Naibu Meya Mariam Dizumba alivyokuwa anaiba kura zilizopigwa za hapana kutoka kwenye sanduku la kura na kuchukua kura za ndiyo kutoka kwenye mkoba wake na kuziweka ndani ya sanduku la kura
Hali hiyo ilisababisha vurugu kubwa na kumfanya Mbunge Dkt Nchimbi akimbie na sanduku la kura kuelekea nje ya ukumbi kabla ya kunyanganywa na kutakiwa kurirudisha ndani na Madiwani wakiongozwa na Madiwani wa Chadema
Wakati Madiwani wanamnyang’anya sanduku la kura Dkt Nchimbi ndipo Naibu Meya Mariam Dizumba alipata mpenyo wa kukimbia na kufanikiwa kuingia ndani ya gari na kutokomea kusikojulikana na kufanya madiwani kuvua majoho na kuondoka zao huku wakimzomea Dkt Nchimbi na kurusha maneno ya matusi
Baada ya tafrani hiyo Madiwani wa Chadema waliitisha kikao na waandishi wa habari na kutoa tamko la kutomtambua Charles Mhagama kuwa Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa hiyo na kwamba wameiomba tume ya uchaguzi ione umuhimu wa kuitisha uchaguzi mwingine
“Akisoma tamko hilo kwa niaba ya madiwani wenzake kwenye ukumbi wa Saccos ya halmashauri hiyo Diwani wa kata ya Bombamabili Kenny Mpangara alisema kuwa mazingira yote ya zoezi la uchaguzi yameonekana na utata kwa maslahi binafsi na kudai kuwa Madiwani wa Chadema watasusia vikao vyote vya halmashauri mpaka Meya mpya atakapopatikana
"Madiwani wa Chadema wapo 7 katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea wakati madiwani wa Ccm wapo 20 ambapo kwenye uchaguzi wa leo walikuwepo 19"alisema Mpangara
Kwa upande wao Madiwani wa Chama cha Mapinduzi wakitoa tamko hilo mbele ya waandishi wa habari na kusomwa na Diwani wa kata ya Lilambo Yobo Mapunda lilisema kitendo walichofanya Madiwani wa Chadema cha kufanya fujo na kutaka kuwapiga wengine ni kitendo kibaya sana katika kukuza demokrasia na kwamba Ccm inamtambua Mstahiki Meya Charles Mhagama
Akizungumza na waandishi wa habari Msimamizi wa uchaguzi Nachoa Zakaria kuhusiana na kitendo cha Naibu Meya Mariam Dizumba kutangaza matokeo badala ya Msimamizi wa uchaguzi alisema kuwa kwenye vikao vya baraza la madiwani Mkurugenzi ni katibu wa vikao na kwamba Naibu Meya ndiye alikuwa sahihi kutangaza matokeo hayo
MWISHO

No comments:

Post a Comment