About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Saturday, September 24, 2011

VIONGOZI WA CHADEMA KUUNGURUMA VIWANJA VYA SOKO LA SAMAKI KUPINGA UCHAKACHUAJI WA UMEYA SONGEA

Joyce Joliga,Songea

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kesho kinatarajia kufanya mkutano mkubwa wa hadhara ili kuwajulisha wananchi vurugu zilizotokea jana wakati wa uchaguzi wa Meya wa manispaa ya Songea na kusababisha uchaguzi kuvurugika kutokana na madai ya kuwepo kwa wizi wa kura.

Akizungumza na mwandishi wa mtandao huu wa http://www.stephanomango.blogspot.com/ na Mwenyekiti wa chama hicho mkoa Joseph Fuime amesema, mkutano huo unatarajiwa kufanyika kesho majira ya saa 9 alasili hadi saa 12:00 katika  uwanja wa soko la Samaki lililopo karibu na shule ya Msingi Mfaranyaki .

Amesema,tayari kila kitu kimeshakamilika na wamepata vibali vya kufanya mkutano huo ambapo viongozi mbali mbali watahudhuria  akiwemo Mbunge wa jimbo la Mbozi Magharibi Silinde pamoja na wakili wa kujitegemea Edson Mbogoro.

Aidha,Fuime ametoa wito kwa wananchi wa Manispaa ya Songea kujitokeza kwa wingi kuhudhuria mkutano huo na tayari mambo yote yamekwenda vizuri na wanatarajia kuwa wananchi watafahamu kila kitu kilichojitokeza kutokana na vurugu hizo.

Kwa Upande wake Katibu wa Chadema Jimbo la Songea Paul Masumbuko amesema,chama kimesikitishwa na vitendo vya vurugu vilivyofanywa wakati wa uchaguzi huo na kueleza kuwa wanaungana mkono na Madiwani wao kutomtambua Mgombea wa umeya ikiwa ni pamoja na kutojishugulisha na shuguli zozote hadi uchaguzi utakaporudiwa.

"Kwanza kwa niaba ya chama  tunapenda kuwapongeza Madiwani wa CCM kwa kuungana na wenzao wa  Chadema ambao wapo  7 katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea wakati madiwani wa Ccm wapo 20 ambapo kwenye uchaguzi wa leo walikuwepo 19"lakini kwa kuonyesha kuwa hawamkubali mgombea wao wamempigia kura za hapana hiyo ndiyo demokrasia ya kweli ", alisema Masumbuko

 Amesema, kitendo kilichofanywa na Madiwani wa CCM kuungana na wenzao wa Chadema kimeonyesha ukomavu mkubwa wa demokrasia na kinapaswa kupongezwa kwa nguvu zote kwani upinzani si kupingana kwa kila kitu bali inapotokea maslahi ya wananchi ni vema waungane na kuonyesha uzalendo mkubwa kwa nchi na wananchi waliowachagua.

Katika tamko lililosomwa  jana na Madiwani wa Chadema  kwa niaba ya madiwani wenzake wa Chadema kwenye ukumbi wa Saccos ya halmashauri hiyo Diwani wa kata ya Bombamabili Kenny Mpangara alisema kuwa mazingira yote ya zoezi la uchaguzi yameonekana na utata kwa maslahi binafsi na kudai kuwa Madiwani wa Chadema watasusia vikao vyote vya halmashauri mpaka Meya mpya atakapopatikana .

Kwa upande wao Madiwani wa Chama cha Mapinduzi wakitoa tamko hilo mbele ya waandishi wa habari na kusomwa na Diwani wa kata ya Lilambo Yobo Mapunda lilisema kitendo walichofanya Madiwani wa Chadema cha kufanya fujo na kutaka kuwapiga wengine ni kitendo kibaya sana katika kukuza demokrasia na kwamba CCm inamtambua Mstahiki Meya kuwa ni Charles Mhagama
MWISHO.

No comments:

Post a Comment