About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Saturday, September 3, 2011



Padre Chinguku ambaye ni Mlezi wa Kituo cha Kulea Watoto Waishio katika Mazingira Magumu SWACCO akiendesha maombi kabla ya Mgeni Rasmi ajaanza kuhutubia Wazazi,Wageni Waalikwa,Wanafunzi na Walimu wa Shule ya Msingi Mkombozi wakati wa Mahafali ya Darasa la Saba katika Shule hiyo



Mgeni Rasmi katika Mahafali ya kwanza ya darasa la saba toka Shule hiyo ianzishwe ,Mhariri Msaidi wa Magazeti ya Elimu na Tujifunze kanda ya Kusini Juma Nyumayo,ambaye alimwakilisha Mhariri Mkuu wa Magazeti hayo Christiani Sikapundwa akiwasalimu wanafunzi na wageni waalikwa kabla hajaanza kuwahutubia,Kushoto ni Diwani wa Kata ya Bombambili kupitia Chadema,Kenny Moto Mpangara,kulia ni Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo,Immelda Mbawala 

                                
Mgeni Rasmi Juma Nyumayo akimkabidhi cheti cha kuhitimu Elimu ya Msingi Mwanafunzi Amina Kazimguru katika mahafali yaliyofanyika jana katika viwanja vya Shule hiyo mjini hapa






No comments:

Post a Comment