About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Saturday, September 3, 2011

 Mzee Samwel Mapunda na Mkewe Mwalimu Notbuluga Mapunda(Mwalimu Bibi) hawakubaki nyuma katika Mahafali hayo kwa kumsindikiza mjukuu wao Dickson Mapunda kushikana mkono na Mgeni Rasmi Nyumayo na kupokea uthibitisho wa kuhitimu elimu ya Msingi darasa la Saba mwaka huu 2011
 Hapa sasa ni kucheza Kiduku kwenda mbele kwa wahitimu wa darasa la saba katika Shule ya Msingi Mkombozi ikiwa ni furaha ya kuhitimu na kukabidhiwa cheti na Mgeni Rasmi Nyumayo kwa kudumu katika darasa la kwanza hadi la saba mwaka huu
 Usiposhuhudia Mahafali haya unaweza kujilaumu kwa kukosa raha na maneno ya busara na hekima kutoka kwa Mgeni rasmi Nyumayo na hapa ni watoto ambao urefu wake ni wa mashaka wakiwa wanatafuta uwezo wa kuona kinachoendelea
 Wageni waalikwa,walimu na wanafunzi wakiwa wanafuatilia mahafali hayo kwa umakini mkubwa
 Mgeni Rasmi Juma Nyumayo ambaye ni Mwanaharakati wa masuala ya haki za binadamu akimpa msaada wa fedha ya kununulia Uniformu Mwanafunzi wa darasa la tano Agnes Magagura baada ya kusikia kuwa anashindwa kuendelea na Shule kwa kukosa Uniformu na kuguswa kutoa msaada huo
Mwalimu Mkuu Mstaafu wa Shule ya Mkombozi Agnes Nkoma akishangiliwa na Wanafunzi wake alipokuwa anawaaga na kwenda kuanza maisha mapya ya URAIANI kwa kuwa amestaafu utumishi wa Umma

No comments:

Post a Comment