About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Tuesday, October 4, 2011

VIONGOZI WA DINI WAOMBWA KUWANUSURU WANAFUNZI WA MTONYA NA MAPEPO

Na Augustino Chindiye,Tunduru

SHULE ya Msingi Mtonya Wilayani Tunduru imefungwa kwa muda usiojulikana ili kuwapisha Wazee wa mila,Mapadre na  Mashehe ili wawasaidie kuomba na kuyaondoa Mapepo ambayo yamekuwa yakisababisha Wanafunzi wanaosoma katika Shule hiyo kupatwa na homa ya kuchanganyikiwa na kuanguka wakati wa masomo.

Amri ya kufungwa kwa Shule hiyo imetolewa na Afisa elimu wa Shule za Msingi Mwl. Rashid Mandoa baada ya juhudi za maafisa tabibu kutoka katika Hospitali ya Wilaya ya Tunduru kushindwa kulitafutia ufumbuzi tatizo hilo.

Mwl. Mandoa aliendelea kufafanua kuwa tatizo la kuanguka na kupoteza fahamu kwa wanafunzi hao limekuwa likiongezeka siku hadi siku ambapo awali idadi ya watoto waliokuwa wakianguka walikuwa ni kati na watoto mmoja na watano lakini hivi sasa tatizo hilo limefikia zaidi ya watoto hamsini kwa siku.

Alisema kufuatia hali hiyo wazazi wa watoto wanaosoma katika shule hiyo walikuwa wakilazimika kufuatana na watoto wao na kupiga kambi pembezoni mwa shule wakiwa na lengo la kuwasaida watoto watakao kumbwa na homa hiyo.

Alisema ingawa Serikali haiamini mambo ya ushirikina lakini idara yake imechukua maamuzi hayo baada ya kubaini kuongezeka kwa matukio hayo na kwamba endepo tatizo hilo litaachiliwa liendelee kuna
hatari ya kushusha kwa taaluma za wanafunzi kutakakosababishwa na kushuka kwa ari ya wanafunzi kutopenda masomo.
Mwisho.

No comments:

Post a Comment