About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Friday, January 27, 2012

ABAKWA NA WATU WATANO NA KUMSABABISHIA KIFO

Na Gideon Mwakanosya,Songea
JESHI la Polisi mkoani  Ruvuma linawasaka watu watano wasiofahamika wakazi wa eneo la Lilambo Manispaa ya Songea kwa tuhuma za kuvamia  na kuingia ndani ya nyumba  kisha kumbaka Mwanamke  mwenye umri wa miaka 20  kwa kupokezana wakati akiwa amelala  na kumsababishia Kifo.
Akizungumza na waandishi wa habari jana ofisini kwake kamanda wa Polisi mkoani Ruvuma Michael Kamuhanda  alisema kuwa tukio hilo lilitokea juzi  majira ya saa nne usiku  kata ya Lilambo nje kidogo ya mji wa Songea.
Amesema,Inadaiwa siku ya tukio  majira ya saa nne usiku watuhumiwa hao walifanya kitendo hicho cha kinyama  na kumsababishia maumivu makali  sehemu nyeti  marehemu  ambaye hata hivyo jina lake limehifadhiwa .
Ameeleza zaidi  kuwa  watuhumiwa hao  inadaiwa baada ya kumfanyia kitendo cha unyama mwanamke huyo walimchukua  toka nyumbani kwake na kwenda kumtupa nje ya nyumba kwenye shamba la migomba  ambapo watu waliokuwa wakipita kwenye eneo hilo walishituka kuona mwili wa marehemu ukiwa umelazwa  katika shamba hilo.
Amefafanua zaidi kuwa mara baada ya wananchi wa kata hiyo kuona mwili huo walitoa taarifa kwa viongozi wa  serikali ya kata  ambao ndio waliotoa taarifa kwenye kituo kikuu cha polisi cha Songea , na kuwa askari polisi wakiwa wameongozana na daktari walifika katika eneo la tukio na kuuchukua kwa ajili ya uchunguzi zaidi ambapo waligundua kuwa sehemu zake za siri zinamchubuko.
Kamanda Kamuhand amesema kuwa wakati Polisi wanaendelea kuwasaka watuhumiwa  bado  inaendelea kufanya uchunguzi zaidi kuhusiana na tukio hilo.
Mwisho.
 

No comments:

Post a Comment