About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Tuesday, January 31, 2012

WAKAMATWA NA KILO 350 ZA BANGI NA KILO 112 ZA MBEGU ZA ZAO HILO

KAMANDA WA POLISI MKOA WA RUVUMA MICHAEL KAMUHANDA

Na, Mwandishi Wetu,Tunduru

KIKOSI maalumu cha Oparesheni zuia uharifu cha Polisi Wilayani
Tunduru Mkoani Ruvuma kimewakama watu watatu kwa tuhuma za kukutwa na kilo 350 za bangi zikiwa tayari kwa ajili yakusafilishwa na kusambazwa sehemu mbalimbali za masoko ya walaji.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma Michael Kamuhanda alisema kuwa
tukio hilo limefanikiwa kufuatia taarifa zilizotolewa na raia wema na kufanikisha kuwanasa watu hao ambao miongoni mwao yumo mtuhumiwa wa usambazaji wa madawa hayo katika sehemu mbali mbali za vijiji vilivyopo Wilayani humo.

Kamuhanda alisema kuwa Sambamba na tukio hilo pia watuhumiwa hao walikutwa na kilo 112 za mbegu za bangi ambazo zinadaiwa pia zilikuwa katika harakati za kusafirishwa zikiwa ni juhudi za wakulima wa zao hilo kujidhatiti hasa kipindi hiki
cha kilimo ili kukidhi mahitaji ya soko lao.

Kamanda Kamuhanda aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Adam Mkwanda
(33), Mkwanda Said (29) wakulima wakazi wa Kijiji cha Mpanji Wilayani humo pamoja na Mfaume Alli Mpwanda mnunuzi na msambazaji wa Bangi mkazi wa Kijiji cha Mchoteka Wilayani hapa.

Kamuhanda alifafanua kuwa katika tukio hilo watuhumiwa hao walikutwa wakiwa wamehifadhi shehene hiyo ya bangi katika maghala ya kuhifadhia chakula kukiwa na viroba 6 vilivyo kuwa vimejazwa madawa hayo vikiwa tayari kwa ajili ya kusafirishwa.

Kufuatia hali hiyo kamanda kamuhanda akatumia nafasi hiyo kutoa wito kwa wananchi kulisaidia jeshi hilo kutoa taarifa za matukio ya uhalifu na kwamba hivi sasa wamejipanga kuhakikisha watoa taarifa wanalindwa zikiwa ni juhudi za kutekeleza kwa vitendo maelekezo ya elimu ya ulinzi shirikishi yanayotolewa na jeshi hilo.

Alisema watuhumiwa hao wanatarajiwa kufikishwa mahakama baada ya kukamilika kwa tatratibu za upelelezi ili sheria
iweze kufuata mkondo wake.

Wakati hayo yakijiri uchunguzi unaonesha kuwa wakulima wengi Wilayani humo wamekuwa wakishawishika kulima zao hilo kutokana na kivutio cha bei ambayo hutolewa na wafanyabiashara wake huku kukiwa na wimbi kubwa la ongezeko la watumiaji wa madawa hayo ambayo hudaiwa kuwapatia stimu.

Kwa mujibu wa uchunguzi huo Debe moja la bangi linauzwa kati ya Tsh.20,000/= na 30,000/=  ikiwa ni tofauti na Bei ya mahindi ambayo debe moja hivi sasa linauzwa kwa bei ya 7,000/=.

Mwisho

No comments:

Post a Comment