About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Tuesday, January 31, 2012

WAKULIMA WA KOROSHO WATAKIWA KUWA NA SUBIRA WAKATI SOKO LA MAZAO YAO LINATAFUTWA

   MKUU WA MKOA WA RUVUMA SAID MWAMBUNGU

Na Augustino Chindiye,Tunduru

WAKULIMA wa Korosho Nchini wametakiwa kuwa na subira wakati serikali ikiendelea kutafuta suluhisho la kudumu la upatikanaji wa soko la uhakika wa zao

Hayo yamesemwa jana na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said
Mwambunmgu wakati akiongea na Madiwanai wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru Mkoani humo na kuongeza kuwa hali hiyo imetokana na Serikali kubaini tatizo la ubabaishaji wa Soko la Mazao hayo katika msimu wa Mwaka 2011/2012 hali inayo tishia wakulima kupata malipo ya pili.

Sambamba na ahadi hiyo pia Mkuu huyo wa Mkoa wa Ruvuma amewaahidi wakulima wa mazo hayo kuwa kauli ya serikali juu ya Suluhisho la kupatikana kwa Soko la uhakika litatolewa katika kikao kitakachoketi February 2 Mwaka huuu Mjini Dodoma  na kuwahushisha Wakuu wa Mikoa Mitano inayao lima Korosho nchini.

Akifafanua taarifa hiyo Mkuu wa Mkoa huyo alisema kuwa kikao hicho ambacho Mgeni Rasmi atakuwa Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika Prof.Jumanne Maghembe, Pia kitawahusiha Maafisa Kilimo wa Mikoa na Wilaya husika, wadau na viongozi wa vyama vya Ushirika katika Wilaya na Mikoa hiyo.

Mwambungu aliitaja Mikoa itayaohusika katika Mkutano huo kuwa ni
Ruvuma, Mtwara, Lindi,Pwani na Morogoro ambayo alidai kuwa pamoja nautekelezaji wa majukumu yao ya kawaida pia kwa pamoja wameapa kutolifumbia macho suala la ubabaishaji wa soko la mazao hayo kutoka kwa wakulima zikiwa ni juhudi za kuwarudishia ari wakulima baada ya kuhakikishiwa upatikanaji wa soko la mazao yao.

Kufuatia kuyumba kwa soko la zao hilo Mkuu wa Mkoa huyo akatumia
nafasi hiyo kuwataka viongozi wa Wilaya ya Tunduru kubuni mikakati mbalimbali ya kuwainua wananachi kwa kuwahimiza Wakulima kulima kwa wingi za la Mpunga na kulitumia kwa chakula na Biashara likiwa ni mbadala wa zao la Korosho.

Alisema Wilaya ya Tunduru ambayo ni kati ya Wilaya tano zilipo Mkoa Ruvuma ni tajiri wa rasilimali ardhi ambayo imesheheni Mito na mabonde yanayo tiririsha maji kipindi cha mwaka mzima na kwamba endapo viongozi watajipanga vyema katika kuwawezesha wakulima kwa kuwawekea miundombinu ya uhakika wataweza kuwaondoa katika mawazo mgando ya utumwa wa kutegema zao moja tu ambalo linaonekana kubezwa na walaji wakati huo wakiwa na mahitaji nalo.

Nao Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Juma Madaha na Mkurugenzi mtendaji
wa Halmashauri hiyo Efraemm Ole Nguyaine walisema kuwa pamoja na
maandalizi ya miundombinu inayoendelea kutekelezwa pia Wilaya hiyo imekwisha jenga Skim 4 za umwagiliaji imenunua matrekta madogo zaidi ya 200 na kuyasambaza katika vikundi vijijini zikiwa ni juhudi za dhati katika utekelezaji wa kauli mbiu ya Kilimo kwanza.

Kwa upande wao baadhi ya Madiwani ambao walitaka majina yao yasitajwe gazetini ambao mbali na kukiomba kikao hicho kutoa kauli yenye maslahi kwa Wakulima walionesha mashaka
makubwa kuwa kikao hicho si lolote kwa madai ya kuwepo kwa fufunu za wanunuzi “kuiweka” kiganjani Serikali hali inayo wafanya kuwa na kiburi cha kuiyumbisha watakavyo huku viongozi wake wakishindwa kutoa kauli.
Mwisho

No comments:

Post a Comment