About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Friday, March 9, 2012

MHANDISI MANYANYA MKUU WA MKOA WA RUKWA ATEMBELEA SHULE YA UFUNDI YA WALEMAVU YOMBO JIJINI DAR ES SALAAM NA KUWATIA MOYO WANAFUNZI HAO

 Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stella Manyanya akisaini kitabu cha wageni kwenye Ofisi ya Mkuu wa Chuo cha Ufundi Yombo mara baada ya kuwasili chuoni hapo
 Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stella Manyanya akiangalia jiko lililotengenezwa na wanafunzi wa chuo cha walemavu Yombo alipotembelea chuoni hapo na hasa katika darasa la wanafunzi wanaojifunza kutengeneza vyuma ambapo jiko hilo alilinunua kwa shilingi elfu ishirini 20000
  Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stella Manyanya akimpongeza Mwanafunzi pekee wa kike Mariam Kamala katika ufundi wa kuunga vyuma chuoni hapo
 Wanafunzi wa ufundi uselemala chuoni hapo wakimuonyesha Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stella Manyanya namna wanavyojifunza ufundi huo
 Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stella Manyanya akikagua mitambo ya ufundi useremala alipotembelea darasa la ufundi huo katika chuo cha Yombo

 Wanafunzi wa Darasa la Ufundi Seremala wakiwa kwenye picha ya pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stella Manyanya alipotembelea chuo hicho
 Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stella Manyanya akiwa kwenye darasa la ufundi kushona

 Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stella Manyanya akiamuangalia Mwanafunzi Catherine alivyokuwa anajifunza kushona nguo
 Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stella Manyanya akiangalia wanafunzi wa Uhazini katika chuo cha Ufundi Yombo
 Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stella Manyanya akiwasalimia wanafunzi wa darasa la Ufundi Umeme katika chuo cha Yombo

 Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stella Manyanya akimuelekeza Mwanafunzi wa Ufundi Umeme Yusuph Said alipotembelea darasa hilo la umeme
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stella Manyanya akiwa kwenye picha ya pamoja na Wanafunzi wa Umeme katika Chuo hicho cha Yombo, ikumbukwe kuwa Mhandisi Stella Manyanya ni msomi na mtaalamu wa ngazi ya juu katika fani ya ufundi umeme na kabla ya kuwa Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Ruvuma na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa alikuwa Injinia wa Shirika la Umeme Nchini Tanzania Tanesco

Chuo cha Ufundi kwa Wanafunzi wenye Ulemavu cha Yombo kinakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo miundombinu, vifaa na mitambo ya ufundi wa kada tofauti, walimu na gharama

Katika ziara yake Mhandisi Manyanya aliwapa moyo wanafunzi hao na kutoa kwa kila darasa shilingi 10000 ambapo jumla ya shilingi elfu tisini 90,000 alizitoa kwenye chuo hicho

No comments:

Post a Comment