About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Thursday, March 29, 2012

WAKULIMA WA KOROSHO TUNDURU BADO HAWAJALIPWA MADAI YAO LICHA YA SERIKALI KUTOA AGIZO

       Mkuu wa wilaya ya Tunduru Juma Madaha
Na Augustino Chindiye, Tunduru

WAKATI kukiwa na maelekezo kutoka Serikani kuwa mabenki yatoe fedha zitakazotumika kuwalipa malipo ya pili, pamoja na kulipia korosho ilizo kopwa kutoka kwa wakulima wa zao hilo wakulima wa wilaya ya Tunduru Mkoani Ruvuma malipo hayo bado hayajaanza  kutolewa.

Hayo yamesemwa na Meneja wa Chama kikuu cha Ushirika wa wakulima wilayani Tunduru (TAMCU) Imani Kalembo alipotakiwa kuzungumzia utekelezaji wa agizo hilo kutoka serikalini.

Akifafanuaa taarifa hiyo Bw. Kalembo alisema kuwa malipo hayo yameendelea kukwama kutokana na majibu ya viongozi wa Benki ya NMB tawi la Tunduru waliodai kuwa bado hawajapokea maelekezo kutoka makao yao makuu juu ya kuanza kutoa fedha hizo zitakazotumika wakati wa malipo hayo.

Katika taarifa hiyo Kalembo alisema kuwa jumla ya tani 4800 zimekwama katika maghala na kusababisha malipo kwa wakulima wa Korosho wilayani humo kushindwa kutolewa ni sehemu ya tani 7000 zilizozalishwa Msimu wa mwaka 2011/2012.

Alisema katika msimu huu Wilaya hiyo ilibahatika kuuza katika mnada mmoja tu kati ya minada 9. ambapo iliuza tani kama 1100 na kwamba hayo ilitokana na wanunuzi wakubwa kukataa kununua korosho hizo kwa bei ya shilingi 1480 kwa kilo moja  waliyoitaka wakulima hao wakiwa wanashinikiza wanunue kwa chini ya shilingi 1400.

Kufuatia hali hiyo baadhi ya vyama vya msingi vya ushirika vya wakulima wa wilaya hiyo vimepata changamoto ya baadhi ya wakulima wake kuondoa korosho maghalani na kuanza kuuza korosho zao kwa walanguzi ambao hutumia kipimo halamu kiitwacho KANGOMBA yaani bakuli linalobeba kilo 2 linanunuliwa kwa shilingi 600.

Akizungumzia hali hiyo Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Juma Madaha pamoja na kuipongeza serikali kwa kutoa tamko hilo alisema kuwa ofisi ya kwa kushirikiana na uongozi wa Mkoa huo zikiwa ni juhudi zaa kuhakikisha kuwa malipo hayo yatolewe kwa haraka.
Mwisho

No comments:

Post a Comment