About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Thursday, September 22, 2011

AZALIWA AKIWA NA UVIMBE KICHWANI NA KUPELEKWA KATIKA HOSPITAL YA MKOA WA SONGEA KWA AJILI YA MATIBABU ZAIDI

 Asante Umbulu mwenye umri wa miezi 3 akiwa amelazwa katika Hospital ya Mkoa ya Songea kwa ajili ya kupata matibabu ya uvimbe wa kichwa,mtoto huyo anatakiwa kupelekwa katika Hospital ya Taifa ya Muhimbili kwa ajili ya matibabu kwani katika Hospital ya Mkoa ya Songea haiwezi kumfanyia Operesheni kutokana na kukosekana kwa vifaa na wataalamu wenye vigezo stahiki

Mtoto huyo anahitaji msaada wa kufika Jijini Dar es Salaam na kupatiwa matibabu,yeyote anayetaka kumsaidia mtoto huyo aende katika Hospital ya Mkoa wa Songea na aonane na DKT NGAIZA kwa maelezo zaidi au piga simu 0755-33 50 51utaunganishwa na Dkt Ngaiza


Waandishi wa habari wakizungumza na mama wa mtoto Asante Umbulu katika Hospital ya mkoa wa Songea,Martina Nombo,kutoka kushoto ni mwandishi wa gazeti la Mwananchi,Joyce Joliga,katika ni Cresencia Kapinga mwandishi wa gazeti la Majira

Mtandao huu wa http://www.stephanomango.blogspot.com/ unatoa pole kwa familia ya Martina Nombo kwa kumuuguza mwanao Asante Umbulu

No comments:

Post a Comment