About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Thursday, September 22, 2011

Maskini mtoto IVVO PONERA anavyoteseka baada ya kuungua moto shambani baada ya kibanda alimukuwepo kuungua moto


 
 Mtoto IVVO PONERA mwenye umri wa mwaka mmoja akiwa amelazwa katika Hospital ya mkoa wa Songea baada ya kufikishwa Hospital hapo akitokea kijijini kwao Mchomolo Wilayani Namtumbo,

Mama wa mtoto huyo Paulina Lwambo akizungumza na mtandao huu wa http://www.stephanomango.blogspot.com/ katika hospital hiyo alisema kuwa IVVO alikuwa analelewa kwenye kibanda shambani na kaka yake aitwaye Jackson Ponera wakati yeye anaendelea na shughuli za kuvuna mahindi

Alisema kuwa katika kibanda hicho alikuwa amepika chakula ili waweze kujipatia mlo baada ya kumaliza kuvuna,ghafla akasikia mwanaye Jackson anamwita huku akisema kibanda kinaungua moto

"Niliacha kuvuna na kukimbilia kwenye kibanda na kukuta kibanda kinaungua na mtoto IVVO yupo ndani,nilichanganyikiwa lakini nilifanikiwa kumuokoa akiwa ameharibika mwili wake kwa kuungua"alisema Lwambo

Alieleza zaidi kuwa nilimchukua kwa umakini mkubwa na kumleta hapa Hospital kwa ajili ya matibabu na anaendelea vizuri na matibabu

No comments:

Post a Comment