About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Thursday, September 22, 2011

MTOTO AZALIWA NA UVIMBE KICHWANI,WENGI WANASEMA HUENDA ANA VICHWA VIWILI

Na Stephano Mango ,Songea

Martina Nombo (27) mkazi wa kijiji cha Lulambo Wilayani Mbinga Mkoani Ruvuma amejifungua Mtoto wa kike ambaye anadaiwa kuwa na vichwa viwili ameomba msaada kwa watu wenye uwezo wamsaidie wakiwemo wataalam wa upasuaji wa Kichwa wamsaidie kuhokoa maisha ya Mwanaye.

Akizungumza na mtandao huu wa www.stephanomango.blogspot.com  katika wodi namba tano  ambapo amelazwa na Mwanaye huyo hospitali ya Mkoa wa Ruvuma jana mara baada ya  kupata rufaa kutoka hospitali ya  Mbuyula iliyopo Wilaya ya Mbinga

 Mama wa Mtoto huyo amesema, alijifungua salama  kwa njia ya kawaida mapema  9 juni mwaka huu katika hospitali ya Mbuyula ambapo mara baada ya kukabidhiwa mwanaye na wauguzi aligundua kuwepo kwa tatizo hilo na aliwaarifu nao walimweleza kuwa aendelee kuwa na subira.

Amesema, tangu alipojifungua katika hospitali ya Mbuyula kichwa cha mtoto waki kilizidi kukua na kutengeneza kitu kama uvimbe ambapo mtoto  aliendelea kutibiwa hospitalini hapo hadi madaktari walipompatia rufaa ya kumwamishia  katika hospitali ya mkoa jana  kwa ajili ya matibabu zaidi.

Kwa upande Daktari Bingwa wa upasuaji wa hospitali hiyo Hassan Lumbe amesema, picha ya  X-ray imeonyesha kuwa ndani ya kichwa kuna shimo ambalo linasababisha ubongo utoke na kuingia kwenye  uvimbe ,pia mifupa ya kichwa aijajiunga vizuri.

Amesema,upasuaji wa mtoto huyo katika hospitali hiyo hauwezi kufanyika  kutokana na kutokuwa na vifaa  na utaalamu walionao hawakidhi viwango vya kutoa tiba kwa mtoto huyo hivyo wanamrufaa kwenda muhimbili .

Amesema,kesi kama hizo ni chache kuripotiwa katika Hospital hiyo na kwamba wao walimpokea  baada ya kupewa rufaa toka katika hospitali aliyozaliwa ya  Mbinga  nao wanatarajia kumpatia rufaa kwenda hospitali ya taifa ya  Mhubili kwani wamefanya vipimo na vimeonyesha kuwa opelesheni hiyo haiwezi kufanywa hapo na wanachofanya ni kuandaa rufaa pamoja na fedha kidogo ya kumsaidia kumsafirisha Mama huyo na Mwanaye.

Mwisho.



No comments:

Post a Comment