About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Thursday, September 22, 2011

WATATU WAFIKISHWA MAHAKAMANI KWA KUITAPELI BENKI YA NMB

Na Gideon Mwakanosya, Songea
WATU watatu wamefikishwa Mahakamani  kwa kosa la kula njama na kutenda kosa la jinai  la kufanya udanganyifu  na kujipatia mkopo wa fedha toka  katika Benki ya NMB tawi la Songea Mkoani Ruvuma .

Wakisomewa shitaka hilo jana na  Hakimu mkazi Mfawidhi Mwandamizi Baptisti Mhelela amesema,washitakiwa  wote kwa pamoja walitenda  kosa hilo  kati ya oktoba 22 mwaka 2008 na desemba  5 mwaka 2010 .

Amesema,katika kosa la pili mshitakiwa namba moja Cosmas Haule (35) anashitakiwa peke yake kwa kujipatia mkopo wa fedha   shilingi milioni arobaini kwa udanganyifu  kati ya kipindi hicho hicho cha oktoba 22 mwaka 2008 na 5 desemba 2010 na aliposomewa kosa alikana.

Amesema,mshitakiwa Cosmas yupo nje kwa dhamana  na  ametoa hati ya nyumba na dhamana ya mali isiyo hamishika yenye thamani ya shilingi milioni kumi pamoja na dhamana ya milioni 15  kesi hiyo inatarajiwa kutajwa septemba 30 mwaka huu,upelelezi bado haujakamilika.

Katika kosa la tatu,Mshitakiwa namba tatu Asha Banda (35) anashitakiwa kwa kosa la kujifanya  mmiliki wa nyumba namba 22 kitalu L L Mateka B wakati ilikuwa siyo jambo la kweli na kubadili jina kuwa anaitwa Consolata Alphonce Soko .

Inadaiwa kuwa mshitakiwa alitenda kosa hilo kati ya tarehe hizo hizo  oktoba 22 ,2008 na 5 desemba 2010 katika benki ya NMB tawi la Songea.

Mshitakiwa amekana shitaka na yupo nje kwa dhamana ya shilingi milioni tano ,na mshitakiwa namba 2 Onesmo Soko  naye yupo nje kwa dhamana  ya milioni tano.
Mwisho.

No comments:

Post a Comment