About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Thursday, September 29, 2011

CHADEMA KUMPINGA MEYA ANAYEDAIWA KUCHAKACHUA MATOKEO YA KITI HICHO TUKUFU

Na  Joseph Mwambije,Songea
CHAMA cha demokrasia na maendeleo(CHADEMA)Mkoani Ruvuma kimepanga kufanya maandamano makubwa ya kupinga uchaguzi wa Meya wa Manispaa ya Songea ulio mwezesha Charles Mhagama kuwa Mstahiki Meya anayedaiwa kuchaguliwa kwa kura za ndiyo 12 na za hapana 14 na kuweka kambi kwenye viwanja vya Manispaa.
 
Hayo yamebainishwa juzi na Mwenyekiti wa Chama hicho wa Mkoa wa Ruvuma Bw. Joseph Fuime wakati akiwahutubia maelfu ya wananchi wa Songea kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya Shule ya msingi mfaranyaki.
 
Alisema kuwa sababu kubwa ya kufanya maandamano hayo ni kupinga uchaguzi huo uliofanyika bila kufuata taratibu na kwamba licha ya kuwa Halmashauri ya Manispaa Songea kuwa maskini lakini wamemchagua Meya aliyedai kuwa ni mwizi.
 
‘Wamemchagulia Meya aliyehusika na uuzaji wa greda kwa shilingi milioni18,ununuzi wa gari  bovu la Zimamoto kwa shilingi milioni 350 ambalo halifanyi kazi na huu ni mpango wa Wabunge kuweka watu wao ili waibe fedha’alisema na kuongeza
 
‘Mlifanya makosa makubwa kumchagua Nchimbi(Emanuel Nchimbi) na mngemchagua Mbogoro(Edson Mbogoro) kuwa  Mbunge wenu  tusingepata Meya mwizi na kama ingekuwa enzi ya Nyerere Nchimbi angejiuzulu anamtka Meya huyo ili amtumie kujinufaisha na tunatamka kuwa huyo si Meya wa wananchi ni Meya wa Mbunge na atapopita mitaani mumzomee’alisema.
 
Alimshambulia Mbunge wa jimbo la Songea Mjini  Emmanuel Nchimbi kuwa hana nia njema na wananchi wake na kwamba watakuwa tayari kutoa ushahidi kuwa kura ziliibwa na hivyo watapambana kwa kutumia  akili na busara na watashinda.
 
Alisema kuwa kabla ya kufanya maandamano hayo watazunguka kata 21 za Manispa ya Songea kufanya mikutano ya kuwahamasisha wananchi kujitokeza kwenye  maandamano na kuanda vyakula na taa na kisha kuvigeuza viwanja vya Manispaa kuwa Viwanja vilivyomng’oa  madarakani aliyekuwa Rais wa Misri.
 
Hata hivyo  Bw. Mhagama alipoulizwa kuhusu tuhuma za kuhusika na ununuzi wa gari bovu la Zimamoto,uuzaji wa greda alisema yeye hausiki na tuhuma hizo kwa kuwa magari hayo yalinunuliwa saba Nchi nzima na kwamba greda liliuzwa kwa kufuata sheria zote.
 
Naye  katibu wa Jimbo la Songea Mjini Bw. Masumbuko Paul alisema kuwa Wabunge wa Mkoa wa Ruvuma wamekuwa mzigo kwa wananchi wao kwa kushindwa kuwatatulia matatizo yao kama tatizo kubwa la umeme na ajira kwa wananchi,alisema kuwa siku za CCM kukaa madarakani zinahesabika.
 
Kwa upande wake Mwenyekiti wa CHADEMA Jimbo la Songea Mjini Idd Abdalah alilaani kukihusisha CHADEMA na udini,ukabila  na urangi na kuwataka Waislamu kuondoa dhana hiyo na kuungana kuiondoa CCM madarakani huku akiwapongeza madiwani wa CCM waliopiga kura za hapana kwa Mhagama.
Mwisho
 




No comments:

Post a Comment