About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Thursday, September 29, 2011

WAJASIRIAMALI WATAKIWA KUTUMIA FURSA ZILIZOPO KUKUZA SHUGHULI ZAO

                    Na Stephano Mango,Songea
WAJASIRIAMALI wa mkoa wa Ruvuma wametakiwa kutumia rasilimali zilizopo mkoani humo katika shughuli zao ili ziweze kuwasaidia kuondokana na umasikini miongoni mwa jamii zinazowazunguka

Wito huo umetolewa jana kwenye viwanja vya NSSF na Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Thomas Oley Sabaya wakati wa uzinduzi wa  mradi wa utafutaji wa masoko na uuzaji wa bidhaa kwa kutumia gari ya dhahabu iliyotolewa kwa wajasiriamali wa mkoa wa Ruvuma kwa ushirikiano wa Chemba ya Wafanyabiashara,Wenye Viwanda na Kilimo(TCCIA) na Wakorea chini ya mradi wa KOICA

Sabaya ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Songea alisema kuwa Mkoa wa Ruvuma una hali ya hewa nzuri ambayo unaweza kuifanyia shughuli yoyote ile ya kijasiliamali hivyo wananchi wanapaswa waitumie fursa hiyo vizuri katika kukuza uchumi wao na wa jamii yote kiujumla

Alisema kuwa imebainika kuwa wajasiliamali ni muhimu sana katika kukuza uchumi endelevu wa nchi lakini wamekuwa wakikabiliwa na changamoto nyingi ambazo tunapaswa kuziondoa ili waweze kuchangia kikamilifu uchumi wan chi yao

Akizungumza kwenye uzinduzi huo Meneja wa Programu ya Wakorea wa Kujitolea Hwang,Jin Yun(Jenne) alisema kuwa mradi huo ni ushirikiano kati ya KOICA na TCCIA Ruvuma wenye dhumuni la kuimarisha mfumo wa utafutaji wa masoko na uuzaji bidhaa kwa kutumia gari katika mkoa wa Ruvuma

Jin Yung alisema kuwa KOICA kupitia Programu ya Korea ya marafiki wa kujitolea wa dunia ambao husambazwa sehemu mbalimbali husaidia kuijengea uwezo miradi midogo iliyopo kwenye taasisi wanazofanyia kazi

‘Katika mradi huu Serikali ya Jamhuri ya Korea Kusini kupitia Shirika la Kimataifa la maendeleo la Korea(KOICA) imetoa msaada wa dola za Kimarekani 29,550 ambapo TCCIA Mkoa wa Ruvuma imechangia dola za Kimarekani 650 katika kukamilisha mradi huu pia napenda kuushukuru uongozi wa TCCIA kwa ushirikiano wanaoutoa kwa Jaehong Cho kwani bila yeye tusingeweza kufanikisha mradi huu”alisema Jin Yung

Awali Mwenyekiti wa TCCIA mkoa wa Ruvuma Mays Mkwembe akitoa utangulizi wa uzinduzi huo alisema kuwa kwa kushirikiana na KOICA tulifanikiwa kuibua mradi huu ambao unazinduriwa ukiwa na lengo la kuwasaidia wajasiliamali katika nyanza ya usafirishaji na uuzaji bidhaa mbalimbali ili ziwafikie wateja kwa urahisi na kwa muda muafaka

Mkwembe alisema kuwa mradi huu utasaidia kutatua changamoto zinazowakabili wajasiriamali kama vile tatizo la usafiri wa bidhaa kwa gharama kubwa pia bila kuwa na gari ya uhakika,tatizo la kutafuta masoko,kuvumisha na kutangaza bidhaa zao

Alifafanua kuwa kazi ya gari la dhahabu itakuwa ni usafirishaji wa bidhaa hadi kwenye soko ambapo muuzaji anahitaji,kuuza bidhaa mbalimbali katika gari,kutangaza na uvumishaji wa bidhaa mahali popote,maonyesho ya bidhaa kupitia gari,kutangaza shughuli mbalimbali za biashara,kukodisha gari kwa shuguli mbalimbali

 Mwenyekiti huyo alisema kuwa taasisi ya TCCIA ilianzishwa mwaka 1998 mkoani Ruvuma ambapo hadi sasa TCCIA iko katika mikoa yote 21 ya Tanzania Bara na kwamba ipo mbele katika kukuza na kuendeleza sekta binafsi katika mkoa wa Ruvuma

Mkwembe alisema kuwa kazi kubwa ya taasisi hiyo ni pamoja na utetezi na ushawishi katika kujenga mazingira vutivu ya kuendeleza sekta binafsi,kujenga mazingira ya mahusiano na majadiliano na Serikali katika kuendeleza dhana ya ubia kati ya sekta binafsi na sekta ya umma

Alizitaja kazi nyingine kuwa ni utoaji wa taarifa za masoko na biashara mbalimbali kwa kupitia kituo cha taarifa,kutoa mafunzo mbalimbali ya kuendeleza biashara na ujasiriamali,utoaji wa hati ya uasili wa bidhaa
MWISHO




No comments:

Post a Comment