About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Tuesday, November 1, 2011

AUAWA KWA MTWANGIO WA NAFAKA AKICHEZA MUZIKI UKUMBINI

                    Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma Michael Kamuhanda
Na Gideon Mwakanosya,Songea
MKAZI mmoja wa Kijiji cha Ruanda kilichopo katika Wilaya ya Mbinga Mkoa wa Ruvuma Afred Milinga (27) amekufa papo hapo baada ya kupigwa kichwani na mchi wa kutwangia nafaka na Festo Mahundi (21) wakati wakiwa kwenye ukumbi wa starehe wakicheza disko.

Akizungumza na Mwandishi wa habari wa mtandao huu wa http://www.stephanomango.blogspot.com/ Gideon Mwakanosya jana ofisini kwake Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa Ruvuma  Naftan Mantamba alisema kuwa tukio hilo lilitokea juzi usiku majira ya saa 2.30 huko kwenye ukumbi wa starehe kijijini hapo.

Alisema kuwa inadaiwa kuwa kabla ya tukio hilo Milinga aliondoka nyumbani kwake na alielekea kwenye kilabu cha pombe za kienyeji ambako baadae alikwenda kwenye ukumbi wa starehe na alifanikiwa kuingia ukumbini humo ambamo alimkuta Mahundi.

Alieleza zaidi kuwa wakiwa kwenye ukumbi huo walianza kuzozana kati ya milinga na Mahundi ambako Mahundi baadae alitoka nje ya ukumbi huo hadi kwenye nyumba ya jirani ambako alichukuwa mchi wa kutwangia nafaka kisha aliingia nao ukumbini na kumpiganao kichwani Milinga na kumsababishia kifo papo hapo.

Mantamba alisema kuwa baada ya kutokea kwa tukio hilo Mahundi alikimbia na kutokomea kusikojulikana lakini baada ya muda Polisi walipopata taarifa ya tukio hilo walifanikiwa kumkamata Mahundi akijiandaa kutaka kukimbia kuelekea kijiji cha Lituhi.

Hata hivyo Mantamba alieleza kuwa chanzo cha tukio hilo ni ugomvi uliotokea kati ya Milinga na Mahundi uliotokea kwenye ukumbi wa starehe ambako kulikuwa na disko na kwamba mtuhumiwa huyo atafikishwa mahakamani mara tu upelelezi utakapo kamilika.

No comments:

Post a Comment