About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Friday, December 9, 2011

WAHITIMU WA VETA KUPEWA KIPAUMBELE CHA AJIRA KWENYE MGODI WA URANI

Mkurugenzi wa  Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi Kanda ya Nyanda za juu kusini Monica Mbelle

Na Joseph Mwambije ,Songea
SERIKALI  Mkoani Ruvuma imesema itatoa kipaumbele  katika kutoa ajira  kwenye mgodi wa madini ya Urani  yanayotarajiwa kuanza  kuchimbwa hivi karibuni kwa Wahitimu wa Chuo cha mafunzo ya ufundi stadi(VETA) cha Songea Mkoani Ruvuma baada ya utafiti wa madini hayo kukamilika.
 
Msimamo huo wa Serikali  ulitolewa juzi na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu kwenye  Mahafali ya 26 ya VETA Songea kupitia hotuba yake iliyosomwa kwa niaba yake na Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo  Saveli Maketa  ambaye aliwataka Wazazi kuwapeleka  watoto wao katika Chuo hicho  na kusema kuwa ukisomea ufundi huwezi kukosa kazi.
 
‘Vyuo vya  mafunzo ya ufundi stadi vina umuhimu mkubwa katika kipindi hiki ambacho ajira zimekuwa zikitatiza lakini pamoja na kusumbua kwa ajira lakini ufundi umekuwa ukiwafanya watu wachomoze na kufanikiwa kimaisha’alisema.
 
Kutokana na umuhimu huo alisema Serikali imepanga kujenga Vyuo vya ufundi stadi kila Wilaya ili kutoa nafasi kwa vijana wengi zaidi kupata ujuzi  na kujiajiri na kwa kujiunga na Vyuo hivyo alisema wanaweza kupambana na umaskini.
 
Aliwataka wahitimu 52 kati yao wavulana 42 na wasichana 10 wa fani za aina mbalimbali waliosoma kwa miaka mitatu Chuoni hapo kwenda kutumia ujuzi walioupata kulijenga Taifa  na kujiunga kwenye Vikundi vya maendeleo na Vyama vya akiba vya kuweka na kukopa(SACCOS) ili waweze kupata mitaji ya kununulia vitendea kazi.
 
Alilisisitiza kuwa  wahitimu wa VETA na Wananchi wa Mkoa wa Ruvuma kwa ujumla watapatiwa kipaumbele kwenye ajira katika mgodi wa Urani uliopo Namtumbo Mkoani humo ambao utakuwa mmoja wa migodi mikubwa duniani na kwamba utafiti wa madini hayo umeshakamilika na yataanza kuchimbwa hivi karibuni.
 
Kwa upande wake Mkurugenzi wa  Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi Kanda ya Nyanda za juu kusini Monica Mbelle aliwataka wazazi kuachana na dhana potofu kwamba ufundi ni kwa wavulana tu na kuwapeleka watato wa kike Chuoni  hapo.
 
Aliwataka wahitimu kwenda kufanya kazi ya kusaidia  jamii na kwamba kwa kutokufanya hivyo watakuwa hawajalitendea haki taifa lao kwa kuwa Serikali imetumia gharama kubwa kutoa mafunzo hayo huku ikitoza pesa kidogo.
 
MWISHO

No comments:

Post a Comment