About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Saturday, October 15, 2011

WAANDISHI WA HABARI KUJADILIANA NA WADAU WA HABARI MKOANI RUVUMA LEO

                            Katibu wa Ruvuma Press Club Andrew Chatwanga
Baadhi ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Ruvuma wakiwa na Waziri wa Habari,Utamaduni na Michezo Dkt Emmanuel Nchimbi
Na Stephano Mango,Songea
CHAMA cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Ruvuma kinatarajia kuanza mkutano wa Wadau wa Habari mkoani Ruvuma ulioandaliwa na chama hicho unaotarajiwa kufanyika kwenye ukumbi wa Chama Cha Walimu Tanzania tawi la Ruvuma(CWT)
Akizungumza kabla ya mkutano huo wa Wadau kuanza Katibu wa Chama Cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Ruvuma Andrew Chatwanga alisema kuwa mkutano huo ambao utafunguliwa na Mgeni rasmi ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu una lengo la kujadili mafanikio na changamoto zinazoikabili sekta ya Habari mkoa wa Ruvuma
Chatwanga alisema kuwa washiriki watapata fursa ya kuelezwa historia fupi ya Chama cha Waandishi wa habari mkoa wa Ruvuma,Utaratibu wa Wadau  kuwapata Waandishi wa Habari,Kuelewa majukumu ya Chama cha Waandishi wa Habari kwa maendeleo ya mkoa wa Ruvuma,Kusuluhisha migogoro baina ya Waandishi wa Habari na Wadau
Alifafanua kuwa mkutano huo ni muhimu sana kwani utawezesha kurahisisha upatikanaji wa habari na ujenzi wa uandishi wenye ueledi kwa maendeleo ya wananchi wote kwa ujumla

No comments:

Post a Comment